Akihutubia mkutano wa jukwaa la usimamizi wa intaneti,IGF,unaofanyika hii leo mjini Paris Ufaransa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, katika miaka 13 tangu mkutano wa kimataifa uliofanyika Tunisia mwaka 2005, dunia ya kidijitali imebadilika kwa kasi, fursa mpya zimefunguka na hivyo masuluhisho ya kidijitali yanabadili maisha ya watu na kwamba yanaweza kusongesha mbele kazi ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.