Wananchi wa Rumbek nchini Sudan Kusini, sasa watahabarika kutwa nzima kila siku, tena kwa kupitia lugha mbalimbali ikiwemo lugha ya mama Dinka, Kiarabu na Kiingereza baada ya Radio pekee ya jamii inayoendeshwa na serikali ya Rumbek 98FM kupigwa jeki na mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS.