Hali ya hatari dhidi ya raia kwenye mji wa Derna Mashariki mwa Libya inazusha wasiwasi mkubwa hasa kuhusu hatma ya raia, kufuatia mapigano yaliyoshika kasi na kundi la jeshi la jeshi la kitaifa nchini humo LNA kuarifu kudhibiti wilaya zilizo na idadi kubwa ya watu.