Nchini Tanzania nako maadhamisho ya siku ya walinda aman iwa Umoja wa Mataifa ambapo imeelezwa kuwa ni siku muhimu kwa kuzingatia kuwa katika miaka 70 ya ulinzi wa amani wa UN, Tanzania imeshiriki operesheni hizo kuanzia mwaka 2006.
Baada ya pande kinzani nchini Sudan Kusini kuridhia sitisho la mapigano, IGAD imezitaka kusimamia ahadi hiyo ili hatimaye kuwepo na amani ya kudumu nchini humo.
Wajumbe na viongozi wa kidini kutoka Sudan Kusini, wanaohudhuria mkutano wa ngazi za juu wa jukwaa la kuongeza matumaini ya amani nchini mwao, wamejikuta wakibubujika machozi kutokana na mateso waliyoshuhudia nchini mwao.
Ifikapo mwaka 2050 inakadiriwa kuwa watu wawili kati ya watatu watakuwa wanaishi mijini kwa mujibu wa ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo, ikiainisha haja ya kuwa na mipango miji endelevu na huduma muhimu za jami.
Nilichokishuhudia Sudan Kusini kwa maelfu ya watu waliotawanywa kinasikitisha, amesema msaidizi wa Katibu Mkuu wa masuala ya kibinadamu Mark Lowcock ambaye leo anahitimisha ziara ya siku mbili nchini humo.
Katika jitidaha za kupambana na unyanyasaji na ukatili wa kingono katika maeneo ya operesheni za Umoja wa Mataifa hasa kuliko na vita , Umoja wa Mataifa umelivalia njuga suala hilo na kuwasaidia waathirika kwa kuzindua mirandi mbalimbali itakayowasaidia.
Idadi ya waliokufa kutokana na athari za mafuriko nchini Kenya imepanda. Ofisi ya shirika la Umoja wa Mataifa inayoratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA linasema kuwa hadi sasa idadi ya waliofariki imefikia watu132 huku zaidi ya 311,000 wameachwa bila makazi.