Ushirikiano kati ya vyombo vya usalama ikiwemo polisi na FRDC ambalo ni Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na vikosi vya walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu chini ya Mwavuli wa MONUSCO, umeendelea kuzaa matunda kwa kuwahakikishia usalama wananchi wa maeneo ya mashariki mwa DRC.