Mkutano wa wajumbe wa jopo la wakaguzi wa nje wa Umoja wa Mataifa ukimalizika leo kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Tanzania ambayo ni mjumbe wa jopo hilo imesema imekuwa ni fursa ya kubadilishana mawazo hususan masuala ya kuepusha mgongano wa maslahi, udanganyifu na rushwa.