Leo Jumamosi, tarehe 26 Machi 2022, Umoja wa Mataifa utashiriki tena katika "Saa ya Dunia", mpango wa kimataifa unaounganisha mamia ya mamilioni ya watu binafsi, makampuni, mashirika na serikali duniani kote kuzima taa zao kuanzia saa mbili na nusu usiku (2:30 usiku) hadi Saa tatu na nusu usiku 93:30 usiku) ili kuzingatia masuluhisho ya watu katika kulinda sayari na kujenga mustakabali mzuri na endelevu.