Bara la afrika limepiga hatua kubwa katika vita dhidi ya janga la COVID-19, idadi ya wagonjwa na vifo inapungua lakini bado kuna changamoto kubwa kuhusu janga hilo limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa na tiba kwa gharama nafuu UNITAID ambalo linajikita katika kutafuta suluhu za kibunifu za kuzuia, kutambua na kutibu magonjwa kwa haraka zaidi katika nchi za kipato cha kati na cha chini.