Zaidi ya siku 100 zimepita tangu Urusi kuvamia Ukraine, na hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametambulisha ripoti ya pili kutoka kikundi cha kuchukua hatua dhidi ya janga la dunia litokanalo la vita hivyo, GCRG na kusema madhara ya vita hiyo katika sekta ya chakula, nishati na fedha ni dhahiri shairi na yanazidi kuongezeka kila uchao.