Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amepokea tamko la mkutano wa nchi 20 zilizoendelea kiuchumi linaloelezea nguzo nne zilizopewa mkazo katika mkutano huo ikiwa ni mustakabali wa kazi, miundombinu ya maendeleo, maendeleo ya chakula endelevu na mkakati wa kuimarisha jinsia kwa kupima matokeo kwa watu wa jinsia tofauti ya sera zilizopangwa katika ajenda ya G20.