Wakati kiwango cha joto kikiendelea kupanda duniani , hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi zinazorota na fursa ya kulishinda jinamizi hili inaendelea kuwa finyu. Jumapili wiki hii Umoja wa Mataifa utaanza majadiliano muhimu ya jinsi gani ya kushughulikia tatizo hilo kwa pamoja na kwa haraka, katika wiki mbili za mkutano wa 24 wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP 24 utakaofanyika mjini Katowice nchini Poland.