Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amesema kuwa mpango wa amani nchini Nepal unaendelea kukumbwa na utata huku Umoja huo ukijiandaa kuondoka nchini humo.
Taarifa ya pamoja iliyotolewa na mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Pakistan balozi Rauf Engin Soysal na mratibu wa Umoja wa Mataifa nchini Pakistan Tomo Pakkala inasema mamilioni ya wapakistan bado wanahitaji msaada kukabili athari za mafuriko yaliyowakumba.
Msimu wa ukame unaendelea kuathiri sehemu kubwa ya Somalia ikiwemo Somalilanda na Puntland limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA.
Kuanzia tarehe 30 Desemba mwaka huu wa 2010 watoto wa nchi ya Congo Brazzaville kutoka jamii ya watu wa asili watapata fursa za masuala ya afya, elimu na kulindwa kutokana na kuwekwa sheria za kuwalinda.
Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR leo limesema litaweka kambi maalumu nchini Liberia ili kuwahifadhi wakimbizi zaidi ya 18,000 waliokimbia machafuko nchini Ivory Coast.
Wataalamu watatu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wamesema wanahofia sana kuendelea kwa ukiukaji wa haki za binadamu nchini Ivory Coast wakati mvutano wa kisiasa ukiendelea.
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP inapeleka kwa kutumia ndege msaada wa chakula nchini Liberia ili kuwalisha maelfu ya watu wanaokimbia mgogoro wa kisiasa katika nchi jirani ya Ivory Coast.
Maafisa wawili wa Umoja wa Mataifa leo wameelezea hofu yao juu ya hali nchini Ivory Coast , na kusema baadhi ya viongozi wanachagiza ghasia na chuki miongoni mwa jamii na kuonya kwamba wanaohusiaka watawajibishwa chini ya sheria za kimataifa.
Bodi ya wakurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP imeidhinisha kuongeza mwaka mmoja zaidi ya mpango wa msaada wa chakula nchini Bangladesh.