Leo ni siku ya kimataifa ya Vesak ambayo ni siku takatifu kwa watu wa dini ya Kibudha siku ambayo inaenzi na kutamini mchango wa dini hiyo katika utamadfuni na Imani.
Mashirika ya kutoa misaada na wadau wa Umoja wa Mataifa, wamelaani vikali kile walichokiita ni mwenendo wa vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wafanyakazi wa misaada, na mashambulizi kwenye matukio mawili yaliyofanywa tarehe 21 Mei mwaka huu nchini Sudan Kusini.
Mkurugenzi mkuu wa shirika la kimataifa la nguvu za atomic IAEA Rafael Mariano Grossi amesema ameafikiana na Iran kuongeza mwezi mmoja zaidi ukaguzi na ufuatiliaji muhimu wa shughuli za nyuklia zinazofanywa na shirika hilo nchini Iran.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amehutubia mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Shirika la afya la Umoja wa Mataifa Ulimwenguni, WHO na kusema iwapo ubaguzi katika utoaji chanjo dhidi ya COVID-19 utaendelea, nchi tajiri zitachanja watu wake wote na kufungua chumi zao huku virusi vikiendelea kusambaa na kubadilika katika nchi maskini na kukwamisha mkwamuko wa uchumi ulimwenguni kote.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa - UN, Antonio Guterres amemchagua Martha Ama Akyaa Pobee kutoka nchini Ghana kuwa msaidizi wake wa Afrika, katika idara masuala ya Siasa, ujenzi wa amani na kulinda amani.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya familia, Umoja wa Mataifa unaangazia umuhimu wa teknolojia katika kuimarisha ustawi wa taasisi hiyo muhimu kwa maendeleo endelevu duniani.
Umoja wa Mataifa leo Alhamisi umewaenzi wafanyikazi 336 waliopoteza maisha yao wakiwa kazini mwaka 2020, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuwahi kutokea kwa mwaka mmoja.
Mfuko wa kimataifa wa chakula endelevu cha samaki (ISSF) Fabien Forget
Zaidi ya tani milioni 6 za samaki Jodari huvuliwa kila mwaka ulimwenguni na aina hii ya samaki inachukua asilimia 20 ya ujazo wa Samaki wote wanaovuliwa wa baharini na kuchangia zaidi ya asilimia 8 ya dagaa zote zinazouzwa duniani umesema Umoja wa Mataifa leo katika siku ya Samaki jodari duniani.