Leo ni siku ya Haki za binadamu, ambapo wito umetolewa kwa kila mmoja kuunga mkono juhudi za kuimarisha usawa kwa kila mtu kila mahali, ili tuweze kupata nafuu bora, ya haki na matumaini mapya pamoja na kujenga upya jamii ambazo ni thabiti na endelevu zaidi katika kujali haki.