Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP limekaribisha ufadhili wa dola milioni 6 kutoka kawa mfuko wa Marekani wa maendeleo ya kimataifa USAID ambao utahakikisha huduma ya misaada kupitia anga, UNHAS inaendelea kwa ajili ya kuwasilisha msaada nchini Jamhuri ya Afrika ya kati, CAR.