Tangu miaka mitano iliopita, UM uliweka kando tarehe 29 Mei kuwa ni siku ya kuadhimishwa rasmi mchango wa wafanyakazi wa kimataifa, waume na wake, wa kutoka kanda mbalimbali za dunia ambao walitumia ujuzi wao, chini ya bendera ya UM, kulinda na kuimarisha amani ya kimataifa, na kuwapunguzia mateso ya hali duni umma wa kimataifa, pamoja na kuendeleza haki za binadamu na kudumisha huduma za maendeleo katika sehemu kadha wa kadha za ulimwengu.