KM Ban Ki-moon amemtumia Raisi wa Baraza la Usalama kwa mwezi Mei, Balozi Zalmay Khalilzad wa Marekani na vile vile Baraza la Usalama la Umoja wa Afrika (AU), ripoti yenye kuelezea, kwa ukamilifu, mfumo wa vikosi vya mseto vya AU na UM vinavyotazamiwa kupelekwa kwenye jimbo la Sudan magharibi la Darfur.