Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi, UNHCR, kwa kushirikiana na serikali ya Sudan, linasema sasa limesajili wakimbizi takribani 10,000 wa Ethiopia ambao wamevuka mpaka mashariki mwa Sudan, na wengine wakiripoti kulazimika kukwepa vikundi vyenye silaha ili kuufikia usalama.