Taarifa ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi imesema watalaam hao wameupokea wito uliotolewa katika mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, wenye mpangilio na unaofuata kanuni za kawaida ambao umepitishwa mjini Marrakesh,Morocco hivi karibuni.
Wito huo umezitaka nchi kushirikiana na sekta binafsi katika kulinda haki za wahamiaji na kuhakikisha wanagawana faida za kiuchumi wanazozalisha.