Kuelekea siku ya kimataifa ya kutokomeza ukwepaji sheria wa vitendo vya uhalifu dhidi ya waandishi wa habari, kesho tarehe pili mwezi Novemba, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, uhuru wa kujieleza na vyombo huru vya habari ni muhimu katika kusongesha na kujenga demokrasia sambamba na kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.