Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, polisi wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA wameendelea kutekeleza wajibu wao wa kulinda raia kwa kushirikiana na vikosi vya usalama vya nchi hiyo ili hatimaye wananchi waweze kuendelea na shughuli zao bila bughudha yoyote.