Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za bindamu, OHCHR, imeelezea wasiwasi wake kufuatia vitendo vya ukamataji wa watu vilivyofanyika wiki iliyopita katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, na pia katika maeneo ya Gondar, Bahir Dar na mengineyo, huku polisi wakitumia vifungu vingi vya hali ya hatari iliyotangazwa tarehe 2 Novemba,2021 ili kukamata, kuwatafuta na kuwaweka kizuizini.