Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO, Dokta Tedros Ghebreyesus ametoa tuzo maalum kwa marehemu Henrietta Lacks mwanamke mmarekani mwenye asili ya Afrika kutokana na seli zake kubadili ulimwengu wa sayansi ya matibabu baada ya kutumika kufanya utafiti wa saratani ya kizazi.