Rais wa Ghana Nana Addo Dankwa Akufo-Addo amehutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 na kusema kuwa kitendo cha matumizi ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 kama kigezo cha uhamiaji kitarudisha nyuma harakati za kupambana na janga hilo.