Mahakama ya rufaa ya mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai, ICC leo imetupilia mbali rufaa ya mwendesha mashtaka wa ICC dhidi ya uamuzi wa mahakama hiyo ya kuwaachi huru rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Laurent Gbagbo na aliyekuwa mkuu wa vijana Charles Blé Goudé.
Umoja wa Mataifa umetoa ripoti leo ukiitaka mamlaka nchini Sudan Kusini kuwawajibisha wanajeshi na viongozi wa kisiasa ambao wanaunga mkono makundi ya jamii yaliyojihami katika eneo la Jonglei ili kuzuia ukatili zaidi.