Katika ujumbe wake kuhusu Siku ya Kupinga Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anakumbusha kwamba migogoro, janga la tabianchi, ukosefu wa usawa na umaskini huwaacha mamilioni ya watu katika hatari ya wahalifu wanaotumia mtandao kuwahadaa waathiriwa kwa ahadi za uwongo.