Bodi ya kimataifa ya kudhibiti madawa ya kulevya (INCB), ambayo ni chombo huru, kinachoungwa mkono na Umoja wa Mataifa, imetoa wito kwa serikali kufanya jitihada zaidi kudhibiti mitandao ya kijamii ambayo inasifu tabia mbaya zinazohusiana na madawa ya kulevya na kuchagiza mauzo ya bidhaa zinazodhibitiwa au kupigwa marufuku.