Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai, ICC, imempata na hatia za jumla ya makosa 61 Dominic Ongwen, kamanda wa zamani wa kundi la Lord’s Resistance Army, LRA la Uganda.
Mwaka 2020 ulikuwa ni mwaka wa majanga lakini 2021 ni mwaka wa fursa na matumaini! Ni kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyotoa leo kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani akielezea vipaumbele vyake 10 kwa mwaka 2021.