Ofisi ya Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu (OHCHR) Ijumatatu imechapisha ripoti mpya juu ya Sudan, ilioeleza ya kwamba mashambulio katili, dhidi ya raia, yalioendelezwa na wapiganaji waasi wa Uganda wa kundi la LRA katika Sudan Kusini, ni vitendo vilivyofananishwa "sawa na makosa ya jinai dhidi ya ubinadamu."