Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, doria inayofanywa kwa ushirikiano wa jeshi la polisi la nchi hiyo, polisi wa Umoja wa Mataifa UNPOL wanaohudumu katika mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo ujulikanao kama MINUSCA inasaidia kuweka utulivu na kukabiliana na uhalifu.