Ikiwa leo ni siku ya kimataifa dhidi ya usafirishaji haramu wa binadamu, Umoja wa Mataifa umepigia chepuo na kuwapongeza wafanyakazi walio mstari wa mbele kusaidia na kunasua watu waliosafirishwa kiharamu hususan wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.