Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo ameelezea hofu yake juu ya kuendelea kwa machafuko yanayosababisha kupotea kwa maisha ya watu nchini Tunisia,na ametoa wito wa kufanyika kwa mazungumzo kwa pande zote ili kumaliza tofauti zao kwa njia ya amani n kurejesha utulivu nchini humo.