Kufuatia kuahirishwa kwa uchaguzi mkuu nchini Libya, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema anatambua tangazo la jana Jumatano tarehe 22 mwezi huu wa Desemba kutoka kwa Kamisheni ya juu ya uchaguzi nchini humo ya kwamba tarehe mpya ya uchaguzi itapangwa na Baraza la Uwakilishi ili awamu ya kwanza ya uchaguzi wa Rais iweze kufanyika.