Hassan Jallow, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) kwenye hoja za kufunga kesi ya Juvenal Rugambarara, aliyekuwa meya wa Kitongoji cha Bicumbi kuanzia 1993-1994, alipendekeza mtuhumiwa huyo ahukumiwe kifungo cha miaka 12 kwa kushiriki kwenye jinai dhidi ya ubinadamu.