Tarehe 16 Oktoba huadhimishwa na Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) pamoja na aila nzima ya UM kuwa ni ‘Siku ya Chakula kwa Wote Duniani’. Siku hii hutumiwa kuwazindua walimwengu ya kwamba watu milioni 854 bado wanaendelea kuteswa na kusumbuliwa, kila siku, na tatizo sugu la njaa na ukosefu wa chakula, idadi ya waathiriwa ambayo inazidi kukithiri kwa sababu ya mifumo dhaifu ya kilimo, ugawaji usiotosheleza wa chakula, uwezo usiofaa wa kuhifadhia chakula, na vile vile kutokana na hali ya vurugu na mapigano, mazingira ambayo hukwamisha huduma za kilimo kwenye maeneo husika.