Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema kutokana na ukata linashindwa kukidhi mahitaji ya wakimbizi na wakimbizi wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na hivyo bila nyongeza ya ufadhili, litalazimika kukata mgao wa fedha na vifaa vya usaidizi kwenye kilimo, uvuvi na ufugaji.