Walinda amani wa kikosi cha 5 cha Tanzania, TANBATT 5 kinachohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaolinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA, wamewatembelea na kuwapelekea zawadi balimbali yakiwemo mavazi, wafungwa wanawake katika gereza la Berberati, mkoa wa Mambelekadei.