Watoto wa kike wenye umri mdogo hata miaka 12 huko Pembe ya Afrika wanalazimishwa kuolewa sambamba na kukeketwa au FGM, katika viwango vya kutisha wakati huu ambapo ukame mkali kuwahi kukumba eneo hilo katika kipindi cha miaka 40 ukisukuma familia katika mazingira magumu, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF.