Shirika la afya duniani kuptia taarifa yake iliyotolewa mjini Cairo Misri, limeonesha wasiwasi mkubwa kuhusu hali ya afya ya binadamu kaskazini mwa Syria ambako watu takribani 200,000 wameyakimbia makazi yao kutokana na ongezeko la operesheni za kijeshi tangu Oktoba 9 na hivyo watu milioni 1.5 wako katika uhitaji mkubwa wa huduma za kiafya.