Baada ya ziara ya siku mbili nchini Malawi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA, Mark Lowcok amesema leo Jumamosi kwamba mgogoro wa chakula nchini humo umeepukwa asante kwa misaada ya kibinadamu iliyotolewa na mvua kubwa iliyonyesha, lakini metoa wito wa hatua madhubuti kuchukuliwa ili kushughulikia miziz ya kutokuwepo kwa uhakika wa chakula inayoathiri mara kwa mara taifa hilo.