Taarifa iliyotolewa hii leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia misaada ya dharura, OCHA imeeleza kuwa Mratibu Mkuu wa misaada ya dharura ya kibinadamu kwenye Umoja wa Mataifa ambaye pia ni mkuu wa, Mark Lowcock, hii leo ameachia dola za kimarekani milioni 25 kutoka mfumo mkuu wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF kwenda kwa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji, IOM ili kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyoko mstari wa mbele katika kutoa hudua ya afya ya kuokoa maisha, huduma za maji na za kujisafi katika mapambano dhidi ya COVID-19 katika Jamhuri ya Afrika ya kati, Haiti, Libya, Sudan Kusini na Sudan.