Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na la mpango wa chakula duniani, WFP leo yameelezea hofu yake dhidi ya kuendelea kwa machafuko kwenye mji wa Hudaydah nchini Yemen na kusema yanaweka njia panda mustakabali wa raia, wakimbizi na operesheni za wahudumu wa misaada ya kibinadamu.