Kadri machafuko yalivyozidi kuenea mwaka 2018, pamoja na idadi kubwa ya watu waliopoteza makazi na kiwango kidogo cha mavuno kilichoambatana na umaskini, hali iliyosababisha idadi ya watu wanaokabiliwa na uhaba wa chakula nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kufikia milioni 13.1, shirika la mpango wa chakula duniani WFP lililazimika kuongeza operesheni zake nchini humo na kufikia watu milioni 5.