Mamia ya watu ambao tayari walizihama nyumba zao kutokana na machafuko Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, wamelazimika kufungasha virago tena baada ya mashambulizi yaliyokatili maisha ya watu kadhaa kwenye kambi walizokuwa wanaishi na kwenye jamii zinazowazungunga, imesema ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharira, OCHA.