Wakimbizi takribani milioni moja wa kabila la Rohingya kutoka Myanmar ambao sasa wamekimbilia Bangladesh kutokana na mateso huko nyumbani , jumapili hii watapa ugeni wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
Hali ya usalama na kibinadamu ikiendelea kuzorota nchini Yemen, hususan mji wa bandari wa Hodeidah, WHO imechukua hatua ili kuhakikisha huduma za afya zinaimarika.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesihi Muungano wa Ulaya, EU, na wanachama wake kuchukua hatua thabiti, za pamoja na za wakati il kuokoa Maisha ya watoto wakimbizi na wahamiaji kabla hawajaingia barani Ulaya.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ana wasiwasi mkubwa kutokana na matukio ya mara kwa mara ya mapigano kati ya wakulima na wafugaji wanaohamahama kwenye maeneo ya Afrika Magharibi na Kati.
Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na UKIMWI -UNAIDS, umekaribisha mchango wa nyongeza wa zaidi ya dola 977,000 kwa ajili ya harakati zake za kupambana na ugonjwa huo.
Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo wamejulishwa kuwa hali ya usalama na kibinadamu nchini Syria inazidi kudorora kutokana na mashambulizi yanayoendelea hivi sasa dhidi ya raia hususan kusini mwa nchi hiyo.
Kamishina mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya wakimbizi Filippo Grandi, ametoa wito kwa matifa wahisani kusaidia kurejesha utulivu katika nchi za Afrika zilizoghubikwa na migogoro.
Kuendelea kushika kasi kwa msimu wa pepo kali na mvua za monsoon kumeongeza shinikizo la mahitaji ya kiafya kwamaelfuya wakimbiz wa Rohingya walioanza kumiminika nchini Bangladesh kwa wingi yapata miezi 10 iliyopita.