Wakati hali ikizidi kuchacha nchini Libya huku makundi ya watu wanaunga mkono utawala wa Muammar Al-Qadhafi ukiwaandamana wakimbizi na kuongeza hali ya wasiwasi juu ya usalama, Umoja wa Mataifa umezidisha nguvu zake ili kuwasaidia makundi makubwa ya wakimbizi wanaomiminika kwenye maeneo ya mipakani pamoja na maeneo ya ndani ya nchi.