Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia masuala ya kibinadamu kwa kuhakikisha msaada wa haraka kwa watu walioathirika na vita na majanga ya asili CERF, mwaka jana ulitenga dola milioni 415 ili kuyawezesha mashirika ya misaada kuwasaidia watu milioni 22 katika nchi 45.