Mwaka 2011 dunia ilitangaziwa kuwepo kwa baa la njaa nchini Somalia ambapo zaidi ya watoto laki 340,000 walikuwa na utapiamlo, na ingawa mwaka huu bado baa la njaa halijatangazwa rasmi nchini humo lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema hali ni tete na watoto zaidi ya laki 380,000 wana utapiamlo mkali ambapo hata ukiwaona watoto hao machozi yatakutoka.