Takribani dola bilioni 1.7 zimechangwa zikiwa ni ahadi kwa ajili ya kunusuru eneo la Sahel ya Kati barani Afrika linalojumuisha nchi za Mali, Burkina Faso na Niger. Mapema leo matarajio yalikuwa kukusanya dola bilioni 2.4
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limesema vita vya silaha na athari za kiuchumi na kijamii zilizosababishwa na janga la corona au COVID-19 vimefanya hali ya Watoto kuwa mbaya zaidi katika ukanda wa Sahel.
Wafanyakazi wa shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM wamesaidia mamlaka za Djibouti katika kusaka na kuzika mabaki ya wahamiaji wanane waliozama mwishoni mwa wiki na kisha miili yao kusombwa hadi fukweni wakati wakitoka Yemen .
Sudan inakabiliwa na zahma mbili kubwa ya mafuriko na mfumuko wa bei kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA.