Watu milioni 19.7, karibu nusu ya idadi ya watu wote wa Afghanistan, wanakabiliwa na njaa kali kulingana na ripoti ya uchambuzi wa hivi karibuni wa tathimini ya hali ya uhakika wa chakula (IPC) iliyofanywa mwezi Januari na Februari 2022 na washirika wa masuala ya uhakika wa chakula na kilimo, ikiwa ni pamoja na shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP na mashirika mengi yasiyo ya kiserikali au NGOs.